PRESHA YA MACHO INAVYOWEZA KUSABABISHA UPOFU.


Na Jacqueline Benson.


PRESHA ya macho ni mingoni mwa maradhi ambayo yanaweza kumsababishia mtu kupata upofu wa kudumu endapo hatapatiwa tiba mapema.
Magonjwa hasa yanayoshambulia mtoto wa jicho na uoni hafifu yanaweza kumuathiri mtu kulingana na mfumo wake wa maisha na umri huku baadhi ya magonjwa kama kisukari na  kisonono  yanachangia maradhi haya kwa kiasi kikubwa na kusababisha ulemavu wa macho.


Ugonjwa wa kisukari pamoja na kisonono huweza kusababisha ugonjwa wa macho na matatizo mengine kutokana na kushusha kinga ya mwili(chembe hai nyeupe) na kutengeneza mazingira rahisi ya mwili kushambuliwa.  Kwa mujibu wa Daktari Bingwa wa magonjwa ya macho na Upasuaji wa retina kutoka Hospitali ya  Agarwal’s  Dar es Salaam, Dk.Emeritus Chibuga alisema kuwa presha ya macho ni ugonjwa unaotokana na kutokuwa na uwiano kwenye mfumo unaotengeneza na kutoa maji  kwenye jicho .
Dkt Emeritus aliongeza kuwa kiasi cha utengenezaji wa maji katika jicho ni wa kawaida ila yanayotoka huwa ni kidogo jambo ambalo husababisha mkandamizo wa retina kutokana na wingi wa maji.Mpaka kufikia hatua ya kuitwa presha ya jicho Dk.Emeritus alieleza kuwa tayari mishipa ya  fahamu unaomwezesha mtu kuona imekwisha kuharibika kutokana na maji maji hayo.



Utengenezaji  wa maji haya ni muhimu kutokana na kusafirisha virutubisho katika seli zilizo ndani ya jicho na kuwezesha upatikanaji wa hewa safi ndani ya macho. Kutokuwepo kwa uwiano wa utengenezaji na utoaji wa maji kunasababishwa na kuziba kwa mirija inayohusika na utoaji wa maji hayo na kupelekea jicho kupoteza uwezo wake wa kuona.

Comments

Popular posts from this blog

POLISI ZANZIBAR WAMSHIKILIA MTUHUMIWA WA ULAWITI